Published On:Alhamisi, 2 Oktoba 2014
Posted by Hisia
RONALDO BADO MABAO MAWILI TU KUMKAMATA RAUL LIGI YA MABINGWA, MESSI ATUPWA HUKO!
BADO
 mabao mawili tu Cristiano Ronaldo afikie idadi ya mabao ya Raul 
anayeongoza kwa kufunga zaidi kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya. 
 Mfalme wa mabao; Nyota wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo amebakiza bao moja kufikia rekodi ya Raul katika Ligi ya Mabingwa Ulaya
Mfalme wa mabao; Nyota wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo amebakiza bao moja kufikia rekodi ya Raul katika Ligi ya Mabingwa Ulaya
Ronaldo
 usiku huu amezidi 'kuisuuza roho' ya kocha wake, Carlo Ancelotti baada 
ya kufunga bao moja katika ushindi wa 2-1 ugenini dhidi ya PFC 
Ludogorets Razgrad.
Wenyeji
 walitangulia kupata bao dakika ya sita kupitia kwa Marcelinho kabla ya 
Cristiano Ronaldo kufunga kwa penalti na Karim Benzema kufunga la 
ushindi kwa Real Madrid.

Mwanasoka
 huyo bora wa dunia sasa anatimiza mabao 69 aliyofunga katika Ligi ya 
Mabingwa Ulaya, mawili nyuma ya Raul aliyefunga mara 71.
Anafunga bao hilo siku moja baada ya kocha Ancelotti kukaririwa akisema "Ni mchezaji bora zaidi niliyewahi kumfundisha,".
Kipenzi
 huyo wa mashabiki wa Manchester United sasa anamzidi kwa bao moja, 
mpinzani wake Lionel Messi wa Barcelona, ambaye ana mabao 68. Ruud van 
Nisterlooy anashika nafasi ya nne kwa mabao yake 56, Thierry Henry 
mwenye mabao 50 ni wa tano, Alfred de Stefano mwenye mabao 49 ni wa 
sita, Andriy Shevchenko mwenye mabao 48 ni wa saba, wakati Eusebio 
mwenye mabao 46 sawa na Filippo Inzaghi wanashika nafasi ya nane. Didier
 Drogba anakamilisha orodha ya wachezaji 10 waliofunga mabao mengi Ligi 
ya Mabingwa kwa mabao yake  42.








 
 
 
 
 
 
