Headlines
Published On:Alhamisi, 11 Septemba 2014
Posted by Hisia

ANGALIA KUFURU HII YA NDEGE MPYA YA WANAMICHEZO, NIKE INASHIRIKI UTENGENEZAJI WAKE

Kampuni moja ya ndege imeamua kutengeneza ndege maalum kwa ajili ya wanamichezo ili kuwasaidia kutokana na uchovu.
Inaaminika wanamichezo wamekuwa katika uchovu mkubwa kutokana na safari nyingi za ndege kwenye klabu ikijumuishwa na timu zao za taifa.
Kutokana na hali hiyo kampuni ya vifaa vya michezo ya Nike imeamua kushirikiana na kampuni hiyo ya ndege ambayo haijatajwa kupata ndege ambayo itakuwa na sehemu maalum kwa ajili ya wanamichezo ambayo itawapunguzia uchovu licha ya safari ndefu.
Imetolewa mfano wachezaji wa Brazil ambao walirejea kwao kuungana na timu yao, halafu ikafunga safari hadi Marekani ilipocheza mechi za kirafiki na sasa watarejea kwenye timu zao Ulaya watasafiri zaidi ya kilomita 8000.
Wachezaji wa Premier League, La Liga, Serie A, Bundesliga ndiyo wanaoongoza kwa safari ndefu.

Ndani ya ndege hiyo kutakuwa kuna sehemu ya kupumzikia, kulala, kucheza michezo mbalimbali na vitu vya aina yake vitakavyopunguza uchovu.
Maana yake wachezaji wa Ligi Kuu Bara (Tanzania), hawatapata nafasi ya kupanda ndege hizo kwa kuwa hata ndege za kawaida tu, ni timu chache labda za Yanga, Simba, Azam FC na Mbeya City zimekuwa zikipata nafasi ya kusafiri kwa ndege za kawaida.
Kingine timu hizo hazina safari ndefu sana kwa kuwa timu ni 14 tu, hivyo kuifanya kila moja kucheza mechi 28 kwa msimu na mechi nyingi zinachezwa jijini Dar.


About the Author

Posted by Hisia on 9/11/2014 07:18:00 AM. Filed under , , . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0. Feel free to leave a response

By Hisia on 9/11/2014 07:18:00 AM. Filed under , , . Follow any responses to the RSS 2.0. Leave a response

0 comments for "ANGALIA KUFURU HII YA NDEGE MPYA YA WANAMICHEZO, NIKE INASHIRIKI UTENGENEZAJI WAKE "

Leave a reply

    Blog Archive